Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 05/2024Mfano

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

SIKU 12 YA 31

Mtu anaposikia kiu anatafuta maji ya kunywa. Akinywa hayo maji, yanakuwa sehemu ya mwili wake. Hapo ndipo anapokuwa na afya njema kwa kunywa maji hayo. Mtunzi wa zaburi hii ana hamu kubwa ya kumwona Mungu. Hata amelinganisha hamu yake na kiu ya mnyama wa porini katika nchi ya ukame. Maadui za huyu Mwimba zaburi wanajaribu kumkatisha tamaa, lakini yeye anaamini Mungu atamhifadhi na kumsaidia. Tafakari ushuhuda katika m.8 na 11:Mchana Bwana ataagiza fadhili zake, na usiku wimbo wake utakuwa nami, ... Nafsi yangu, kwa nini kuinama, na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; kwa maana nitakuja kumsifu Aliye afya ya uso wangu, na Mungu wangu. Ni heri kila mmoja wetu awe na kiu ya namna hii.

siku 11siku 13

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 05/2024

Soma Biblia Kila Siku 05/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa tano pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka, Yoeli na Mathayo. Karibu kujiunga na mpango huu

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://www.somabiblia.or.tz/

Mipango inayo husiana