Maelezo ya mpango
Soma Biblia Kila Siku Julai 2021Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Julai 2021](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F26577%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Mji wa Yerusalemu ulitekwa mwaka 586 k.K. Usiku kabla habari hiyo haijafikia Babeli alipokuwepo Ezekieli, neno la Mungu tulilolisoma lilimfikia. Ezekieli alipotabiri juu ya Yerusalemu, ujumbe huo haukupokelewa. Sasa taarifa ya kutimia kwa unabii wa Ezekieli inapowafikia Waisraeli wanaoishi huko Babeli, wanaanza kuhimizana kufika kwa Ezekieli ili kumsikiliza. Wanafika kwa wingi – lakini hawayatendi (m.31, 32) maneno anayowapa Nabii. Tuwe wasikiaji na watendaji wa Neno, tukikumbuka Yesu analosema katika Yn 8:31-32, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Julai 2021](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F26577%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Julai 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu k...
More
Tungependa kuishukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz