Soma Biblia Kila Siku Mei 2021Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Mei 2021](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F25588%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Neno hili laweza kutufundisha mambo mawili. Kwanza ni utii kwa neno litokalo kinywani mwa Mungu. Ijapokuwa marafiki waliomtaabisha Ayubu walimhuzunisha, Mungu alipomtaka Ayubu awaombee, Ayubu alitii. Utii kwa neno la Mungu ni sharti la Biblia. Jambo la pili ni kuwaombea waliotukosea. Hili nalo ni takwa la kimungu na kutusaidia kushinda mafarakano. Yesu asema: Nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi, wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi (Lk 6:27-28). Mambo haya mawili yalikuwa msingi wa Ayubu kurejeshewa ufanisi, uliokuwa umepotea. Kumbuka mambo haya na kuyaishi siku zote.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Mei 2021](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F25588%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Mei 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Tungependa Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz