Soma Biblia Kila Siku 8Mfano

Ahadi inatolewa kwamba siku za mwisho Israeli itarejea makwao wa nguvu za Mungu wakitoka huko uhamishoni (m.3-5: Ndipo Bwana, Mungu wako, atakapougeuza utumwa wako, naye atakuhurumia, tena atarejea na kukukusanya kutoka mataifa yote, huko alikokutawanyia Bwana, Mungu wako. Watu wako waliotawanyika wakiwako katika ncha za mbingu za mwisho, kutoka huko atakukusanya Bwana, Mungu wako; kutoka huko atakutwaa; atakuleta Bwana, Mungu wako, uingie nchi waliyomiliki baba zako, nawe utaimiliki; naye atakutendea mema, na kukufanya uwe watu wengi kuliko baba zako). Lakini lengo la Mungu si kuwakusanya tu kutoka katika mataifa, ila ni kuhakikisha kwamba sasa watamtegemea na kumwabudu yeye peke yake. Lakini ili jambo hili liweze kufanyika lazima Mungu afanye tohara ya kiroho ya mioyo yao; BWANA atautahiri moyo wako, na moyo wa uzao wako, ili umpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, upate kuwa hai (m.6).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 8 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku hasa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Kumbukumbu la Torati, na Yohana pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12

Soma Biblia Kila Siku 9

MWANGA Kuvutiwa Maishani Na Mwanga Ajabu Wa Mungu

Soma Biblia Kila Siku 06/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku 11
