Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 5Mfano

Soma Biblia Kila Siku 5

SIKU 19 YA 31

Asafu, mtunzi wa zaburi hii, alimcha Mungu, tena aliongoza kwaya katika ukoo wa Walawi. Lakini ilimchanganya kuona waovu wakifanikiwa kuliko mtu wa Mungu. Hilo lilimfanya ajiulize maswali mengi. Jaribu hili lilitaka kumrudisha nyuma kiimani (m.2-3). Asafu alifikiri, wema wa Mungu ni kwa wacha Mungu na si vinginevyo (m.1). Tatizo la Asafu linatupata Wakristo wengi. Lakini leo tunafundishwa kuwa wema wa Mungu hauna mipaka (Baba yenu aliye mbinguni ... huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki; Mt 5:45). Sisi Wakristo tuwaombee mema wasiomcha Mungu ili wema wake uwavute wapate kutubu.

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 5

Soma Biblia Kila Siku 5 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/