Zaburi 72:1-4
Zaburi 72:1-4 BHN
Ee Mungu, umjalie mfalme uamuzi wako, umpe mwanamfalme uadilifu wako; atawale taifa lako kwa haki, na maskini wako kwa uadilifu. Milima ilete fanaka kwa watu wako, vilima vijae uadilifu. Mfalme awatetee wanyonge wa taifa, awasaidie watoto wa fukara, na kuwaangamiza watu wadhalimu.