Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 72

72
Kumwombea mfalme
(Zaburi ya Solomoni)
1Ee Mungu, umjalie mfalme uamuzi wako,
umpe mwanamfalme uadilifu wako;
2atawale taifa lako kwa haki,
na maskini wako kwa uadilifu.
3Milima ilete fanaka kwa watu wako,
vilima vijae uadilifu.
4Mfalme awatetee wanyonge wa taifa,
awasaidie watoto wa fukara,
na kuwaangamiza watu wadhalimu.
5Mfalme aishi muda mrefu kama jua,
na kama mwezi, kwa vizazi vyote.
6Awe kama manyunyu yaburudishayo mashamba,
kama mvua iinyweshayo ardhi.
7Uadilifu ustawi maisha yake yote,
na amani kwa wingi mpaka mwezi ukome.
8Atawale kutoka bahari hata bahari,
kutoka mto Eufrate hata mipaka ya dunia.
9Maadui zake wakaao nyikani wanyenyekee mbele yake,
washindani wake walambe vumbi.
10Wafalme wa Tarshishi na visiwa wamlipe kodi,
wafalme wa Sheba na Seba wamletee zawadi.
11Wafalme wote wa dunia wamheshimu,
watu wa mataifa yote wamtumikie.
12Anamkomboa fukara anayemwomba,
na maskini asiye na wa kumsaidia.
13Anawahurumia watu dhaifu na fukara,
anayaokoa maisha yao wenye shida.
14Anawatoa katika udhalimu na ukatili,
maana maisha yao ni ya thamani kubwa kwake.
15Mfalme na aishi maisha marefu;
apokee zawadi ya dhahabu kutoka Sheba;
watu wamwombee kwa Mungu daima,
na kumtakia baraka mchana kutwa.
16Nchi na izae nafaka kwa wingi,
vilima vijae mavuno kama ya Lebanoni,
na watu mijini wastawi kama nyasi.
17Jina la mfalme litukuke daima;
fahari yake idumu pindi liangazapo jua.
Kwake mataifa yote yabarikiwe;
watu wote wamwite mbarikiwa!
18Atukuzwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli,
ambaye peke yake hufanya miujiza.
19Jina lake tukufu na litukuzwe milele;
utukufu wake ujae ulimwenguni kote!
Amina, Amina!
20Mwisho wa sala za Daudi, mwana wa Yese.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 72: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia