Zab 72:1-4
Zab 72:1-4 SUV
Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako, Na mwana wa mfalme haki yako. Atawaamua watu wako kwa haki, Na watu wako walioonewa kwa hukumu. Milima itawazalia watu amani, Na vilima navyo kwa haki. Atawahukumu walioonewa wa watu, Atawaokoa wahitaji, atamseta mwenye kuonea.