1
Warumi 12:2
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
Msifuatishe tena mfano wa ulimwengu huu, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Ndipo mtaweza kujaribu ili kuthibitisha mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yanayopendeza na kamilifu machoni pake.
Linganisha
Chunguza Warumi 12:2
2
Warumi 12:1
Kwa hiyo, ndugu zangu, nawasihi kwa rehema zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu na inayompendeza Mungu, hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
Chunguza Warumi 12:1
3
Warumi 12:12
Kuweni na furaha katika tumaini, katika dhiki kuweni na saburi, dumuni katika maombi.
Chunguza Warumi 12:12
4
Warumi 12:21
Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.
Chunguza Warumi 12:21
5
Warumi 12:10
Pendaneni ninyi kwa ninyi kwa upendo wa ndugu. Waheshimuni na kuwatanguliza wengine.
Chunguza Warumi 12:10
6
Warumi 12:9
Upendo lazima usiwe na unafiki. Chukieni lililo ovu, shikamaneni na lililo jema.
Chunguza Warumi 12:9
7
Warumi 12:18
Ikiwezekana, kwa upande wenu kaeni kwa amani na watu wote.
Chunguza Warumi 12:18
8
Warumi 12:19
Wapendwa, msilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa: “Ni juu yangu kulipiza kisasi, nitalipiza,” asema Mwenyezi Mungu.
Chunguza Warumi 12:19
9
Warumi 12:11
Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana Isa.
Chunguza Warumi 12:11
10
Warumi 12:3
Kwa ajili ya neema niliyopewa nawaambia kila mmoja miongoni mwenu, asijidhanie kuwa bora kuliko impasavyo, bali afikiri kwa busara kwa kulingana na kipimo cha imani Mungu aliyompa.
Chunguza Warumi 12:3
11
Warumi 12:17
Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Jitahidini ili mtende yaliyo mema machoni pa watu wote.
Chunguza Warumi 12:17
12
Warumi 12:16
Kaeni kwa amani ninyi kwa ninyi. Msijivune, bali mwe tayari kushirikiana na wanyonge. Wala msiwe watu wenye kujivuna kwamba mnajua kila kitu.
Chunguza Warumi 12:16
13
Warumi 12:20
Badala yake: “Kama adui yako ana njaa, mlishe; kama ana kiu, mpe kinywaji. Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake.”
Chunguza Warumi 12:20
14
Warumi 12:14-15
Wabarikini wale wanaowatesa, barikini wala msilaani. Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wale waliao.
Chunguza Warumi 12:14-15
15
Warumi 12:13
Changieni katika mahitaji ya watakatifu, wakaribisheni wageni.
Chunguza Warumi 12:13
16
Warumi 12:4-5
Kama vile katika mwili mmoja tulivyo na viungo vingi, navyo viungo vyote havina kazi moja, vivyo hivyo na sisi tulio wengi, tu mwili mmoja katika Al-Masihi, nasi kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
Chunguza Warumi 12:4-5
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video