Soma Biblia Kila Siku Julai 2021Sample
Kazi ya uchungaji siyo mali ya hao wachungaji wenyewe. Ni mali ya Mungu, na inabidi itendeke kwa mapenzi yake. Viongozi wa Israeli walitakiwa kutunza watu wa kundi lao. Badala yake, waliwanyonya ili kujinufaisha kwa faida yao. Hata waliruhusu watu kushambuliwa na kutawanywa na maadui. Kwa kuwa Mungu ni mchungaji mwema, anasema, Mimi mwenyewe nitawatafuta kondoo wangu na kuwatunza (m.11 BHN). Atawakomboa na kuwarudisha kwake. Basi, tukubali kuongozwa na huyo Mchungaji Mwema, ambaye ni sawa na Yesu. Kumbuka anavyojitambulisha katika Yn 10:11, Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
Scripture
About this Plan
Soma Biblia Kila Siku Julai 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More