Soma Biblia Kila Siku Julai 2021Sample
Mungu ndiye Mungu wa faraja yote (2 Kor 1:3). Ndivyo tuonavyo katika somo la leo. Waisraeli wako uhamishoni huko Babeli, na baadhi ya mataifa jirani wamejigawia nchi walimokaa. Lakini nchi hiyo ni mali yake Mungu, wala hatavumilia dharau za maadui hao. Kupitia unabii juu ya milima ya Israeli, Nabii anawahakikishia Waisraeli wamtegemee Mungu. Atageuza kabisa hali hiyo mbaya, na itakuwa njema. Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme (Lk 12:32).
Scripture
About this Plan
Soma Biblia Kila Siku Julai 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More