YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021Sample

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

DAY 16 OF 31

Sote tumeitwa kutenda haki na huruma. Lakini Waedomu walifanya tofauti. Ni ndugu wa Waisraeli, wote wakiwa watoto wa Isaka. Na Waedomu walikula njama na Waisraeli dhidi ya mfalme wa Babeli (Yer 27:3, Jifanyizie vifungo na nira, ukajivike shingoni; kisha uvipeleke kwa mfalme wa Edomu, na mfalme wa Moabu, na mfalme wa wana wa Amoni, na mfalme wa Tiro, na mfalme wa Sidoni, kwa mikono ya wajumbe watakaofika Yerusalemu kwa Sedekia, mfalme wa Yuda). Lakini baadaye, Wababeli walipoangamiza Yerusalemu, Waedomu waliwatoa tu ndugu zao, tena kwa lengo baya la kumiliki nchi yao. Walijua ni kushindana na Mungu wa agano na Israeli (taz. m.10, Umesema, Mataifa haya mawili na nchi hizi mbili zitakuwa zangu, nasi tutazimiliki, ijapokuwa Bwana alikuwako huko), hata hivyo walifanya! Hukumu ya Mungu juu ya Edomu itukumbushe kutoiga mfano wao mbaya.

Day 15Day 17