YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 13

13
Sala ya ukombozi kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 # Kum 31:17; Ayu 13:24; Zab 22:1; Isa 59:2 Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele?
Hadi lini utanificha uso wako?
2Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini,
Nikihuzunika moyoni mchana kutwa?
Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini?
3 # Ezr 9:8; Zab 18:28; Lk 2:32; Ufu 21:23; Zab 76:5,6; Isa 37:36; Yer 51:39; Efe 5:14 Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie;
Uyatie nuru macho yangu,
Nisije nikalala usingizi wa mauti.
4Adui yangu asije akasema, Nimemshinda;
Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.
5 # 2 Nya 20:12 Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako;
Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.
6Naam, nitamwimbia BWANA,
Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

Currently Selected:

Zaburi 13: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy