YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 14

14
Kushutumiwa kwa wasiomwamini Mungu
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 # Rum 3:10-12; Zab 10:4; Mit 1:7,22; Mwa 6:12 Mpumbavu husema moyoni, Hakuna Mungu;
Wameharibu matendo yao na kuyafanya chukizo,
Hakuna atendaye mema.
2Toka mbinguni BWANA aliwachungulia wanadamu,
Aone kama yuko mtu mwenye hekima,
Amtafutaye Mungu.
3Wote wamepotoka, wameoza wote pamoja,
Hakuna atendaye mema,
La! Hata mmoja.
4Je! Wote wafanyao maovu hawajui?
Walao watu wangu kama walavyo mkate,
Hawamwiti BWANA.
5Hapo ndipo waovu watakaposhikwa na hofu nyingi,
Maana Mungu yupo pamoja na kizazi cha haki.
6Mnaiharibu mipango ya mtu mnyonge,
Bali BWANA ndiye aliye kimbilio lake.
7Laiti wokovu wa Israeli ungetoka katika Sayuni!
BWANA awarudishapo wafungwa wa watu wake;
Yakobo atashangilia,
Israeli atafurahi.

Currently Selected:

Zaburi 14: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in