Yesu Ni Nani?Mfano

Yeye ndiye Imanueli.
'Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli. ' (Yohana 1:14).
Ni Krismasi nasi tuna mengi ya kusherehekea!
Mungu yuko pamoja nasi – Yeye ndiye Imanueli.
Katika Yohana 1:14, twasoma kwamba ‘Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu...’ Tafsiri nyingine ya Biblia ya (The New Christian Version) kifungu hicho hicho inasema hivi: ‘Neno likawa mwanadamuna akaishi kati yetu.’
Mungu akawa mwanadamu – mwili na damu. Kwa miaka thelathini na mitatu aliishi kama mwanadamu duniani, anayasikia yote ambayo wewe na mimi tunayasikia. Wanafunzi wa mwanzo walimuona na wakasikia kutoka kwenye mdomo wake yale aliyotaka kufundisha. Alikuwa wa kweli na binafsi, hakuwa wa kudhania na wa kutoka kijijini, hakuwa wa mbali au asiyejali.
Huyu ndiye Mungu wetu wa milele, awezaye kuwafikia wanadamu na hayuko mbali nasi watu wa kawaida. Huyu ndiye Mungu wetu wa milele, yeye ambaye inawezekana kumgusa, mwenye uso wenye hali ya mwanadamu hapa na sasa. Kuzaliwa huku kwa Yesu, ni utimilifu wa unabii uliotamkwa mapema na Isaya miaka mamia kabla. Mungu amekuwa mwanadamu.!
Inaonekana kuwa vigumu kwetu kufahamu ukubwa wa zawadi kwa kila mmoja wetu. Kufahamu kikamilifu kiwango cha neema hii, upendo huu kwa wanadamu. Mungu yuko pamoja nasi.
Hata leo, watu wanapopambana kuelewa Mungu ni nani na Mungu yukoje, tuna uhakika kupitia kwa neno lake na kupitia kwa uzoefu wetu naye kwamba tunaweza kumnyooshea kidole na kusema, ‘Huyu hapa’!
Katika siku hii ya Krismasi, tunatambua ukweli kwamba Mungu yuko pamoja nasi – haijalishi tunakabiliana na nini, popote tulipo, uwepo wake upo pamoja nasi. Tunaposherehekea kuzaliwa kwa Mwokozi wetu, Imanueli, Mungu pamoja nasi, naomba tuungane na Mtume Paulo kutangaza:
‘Mungu ashukuriwe kwa sababu ya kipawa chake, tusichoweza kukisifu kama ipasavyo!’
(2 Wakorintho 9:15)
Tunapokea zawadi ambayo hatungeweza kulipwa wala hatungeweza kustahili – ni zawadi kutoka kwa Mungu ya kupita kiasi namna gani.
Ni kwa njia zipi ukweli kwamba Mungu yuko pamoja nasi unakuhimiza na kubariki maisha yako?
-
Mungu Baba
Leo, tunaungana na Wakristo duniani kote kusherehekea kuzaliwa kwa Mwokozi wetu Yesu. Aliingia katika dunia yetu sio kama mwanadamu bali kama mwanadamu.
Asante kwa zawadi hii isiyoweza kuelezeka.
Tunakiri neema na upendo wako kwa kila mmoja wetu.
Tusaidie kuishi kila siku tukitambua kwamba upo pamoja nasi na kwamba katika chochote tunachoweza kuwa tunakabiliana nacho, tutambue uwepo wako, nguvu na uwezo wako.
Amina
Kuhusu Mpango huu

Tunapoingia Ujio, tukisubiri na kujiandaa kusherehekea kuzaliwa kwa Yesu, tukiiandaa mioyo yetu kwa ajili ya Krismasi, maneno ya Mtakatifu Yohana yanatutangazia hali ya uungu na uwepo wa milele wa Yesu, aliyekuja ‘kusimamisha hema lake’ kati yetu.
More
Tungependa kumshukuru The Salvation Army International kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://salvationarmy.org