Soma Biblia Kila Siku Januari/2022Mfano
![Soma Biblia Kila Siku Januari/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F29514%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Isaka alipomwoa Rebeka alikuwa na miaka 40. Lakini ikapita miaka 20 mpaka Rebeka akamzalia watoto, yaani, Esau na Yakobo (m.26, Isaka alikuwa mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa). Hata hivyo Isaka akawa mwaminifu kwa mke wake miaka yote hii. Badala ya kumlaumu, akazidi kumpenda. Akamshirikisha Mungu tatizo la Rebeka: Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia (m.21)! Je, msomaji, wewe ni mwaminifu kwa mwenzako na kumwombea kwa Mungu katika matatizo yake? Kuwa mwaminifu ni pamoja na kumpenda mwenzako na kumheshimu. Hivi ndivyo inavyompasa mkristo, yaani, ... kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe (Efe 5:21-33).
Andiko
Kuhusu Mpango huu
![Soma Biblia Kila Siku Januari/2022](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2Fhttps%3A%2F%2Fs3.amazonaws.com%2Fyvplans%2F29514%2F1280x720.jpg&w=3840&q=75)
Soma Biblia Kila Siku Januari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Januari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa situ husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Mwanzo. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure.
More
Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/