Soma Biblia Kila Siku 10Mfano

Bwana ni nguvu ya watu wake, maana kwao ni mwamba(m.1), ngao(m.7) na ngome ya wokovu(m.8), yaani mahali pa kukimbilia ili wasife. Hili ni hitimisho la Mwimba Zaburi juu ya msaada wa Mungu kwa wanaomtumainia. Yeye mwenyewe alipomwita Mungu na kuomba msaada wake, alisikilizwa: Ameisikia sauti ya dua yangu(m.6). Mungu huwapatiliza waovu sawasawa na uovu wao, naye atawavunja wala hatawajenga(m.5). Lakini Mungu hawanyamalii wamwitao, wala hawajumlishi wamtumainiao pamoja na wasio haki. Je, wewe unatumania na kutegemea nini katika maisha yako? Tafakari m.7, na fanya kama Mwimba Zaburi: Mtumainie Mungu! Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu. Moyo wangu umemtumaini, nami nimesaidiwa; basi, moyo wangu unashangilia, na kwa wimbo wangu nitamshukuru.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku 10/2020

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku 07/2020

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021
