Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Soma Biblia Kila Siku 10Mfano

Soma Biblia Kila Siku 10

SIKU 14 YA 31

Naye Sauli akamwoza Mikali, binti yake. Sauli akaona na kutambua ya kwamba Bwana alikuwa pamoja na Daudi; na huyo Mikali, binti Sauli, akampenda. Naye Sauli akazidi kumwogopa Daudi; Sauli akawa adui yake Daudi siku zote (m.27-29). Ilikuwa ni ahadi ya mfalme kwamba mtu yule atakayemwua Goliathi atapewa binti wa mfalme kama mke wake. Ila binti wa kwanza wa mfalme alishaolewa na mtu mwingine:Ikawa, wakati ule, ilipopasa Daudi apewe Merabu, binti Sauli, aliolewa na Adrieli, Mmeholathi (m.19). Hii ilikuwa ni bahati yake Daudi, maana binti wa pili wa mfalme, Mikali, ndiye aliyempenda (m.20)! Upendo wake huu alionyesha wazi kwa vitendo wakati Sauli, baba yake, alipotaka kumwua Daudi: Kisha Sauli akatuma wajumbe mpaka nyumbani kwa Daudi, ili wamvizie na kumwua asubuhi; naye Mikali, mkewe Daudi, akamwambia, akasema, Wewe usipojiponya nafsi yako usiku huu, kesho utauawa. Basi Mikali akamtelemsha Daudi dirishani; naye akaenda akakimbia na kuokoka(19:11-12).

siku 13siku 15

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku 10 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Warumi na 1 Samweli.

More

Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz