Soma Biblia Kila Siku 6Mfano
Tafakari maneno haya pamoja na Sefania 2:3, Mtafuteni Bwana, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya Bwana. Tunaitwa kumtafuta Mungu kila siku ya maisha yetu kwa kutega sikio letu kusikia neno lake ili atushikie hatua za mienendo yetu. Tukiweka bidii katika jambo hili, Mungu atatufinyanga upya tupate kipawa cha kumcha na kutushikamanisha naye. Ufahamu ulio bora ni ule unaomwelekea Mungu. Kwa hiyo wito wa leo ni kuweka bidii katika kumtafuta Mungu. Fanya hivyo kwa kuomba na kujifunza Neno lake kwa bidii. Hivyo utaongezeka maarifa ya kumwishi Mungu!
Andiko
Kuhusu Mpango huu
Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz