Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 86:1-7

Zaburi 86:1-7 BHN

Unitegee sikio, ee Mwenyezi-Mungu, unijibu, maana mimi ni fukara na mnyonge. Uyahifadhi maisha yangu maana mimi ni mchaji wako; uniokoe mimi mtumishi wako ninayekutegemea. Wewe ni Mungu wangu; basi, unionee huruma, maana nakulilia mchana kutwa. Uifurahishe roho yangu mimi mtumishi wako, maana sala zangu nazielekeza kwako ee Bwana. Wewe, ee Bwana, u mwema na mwenye kusamehe; mwingi wa fadhili kwa wote wakuombao. Ee Mwenyezi-Mungu, uitegee sikio sala yangu; ukisikie kilio cha ombi langu. Siku za taabu nakuita, maana wewe waniitikia.

Soma Zaburi 86