Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 86:1-7

Zaburi 86:1-7 NEN

Ee BWANA, sikia na unijibu, kwa maana mimi ni maskini na mhitaji. Linda maisha yangu, kwa maana nimejiweka kwako, wewe ni Mungu wangu, mwokoe mtumishi wako anayekutumaini. Ee BWANA, nihurumie mimi, kwa maana ninakuita mchana kutwa. Mpe mtumishi wako furaha, kwa kuwa kwako wewe, Ee BWANA, ninainua nafsi yangu. Ee BWANA, wewe ni mwema na mwenye kusamehe, umejaa upendo kwa wote wakuitao. Ee BWANA, sikia maombi yangu, sikiliza kilio changu unihurumie. Katika siku ya shida yangu nitakuita, kwa maana wewe utanijibu.