Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 141

141
Hatari za tamaa mbaya
(Zaburi ya Daudi)
1Nakuita, ee Mwenyezi-Mungu,
uje haraka kunisaidia!
Uisikilize sauti yangu wakati ninapokuita!
2 # Taz Ufu 5:8 Sala yangu uipokee kama ubani;
niinuapo mikono yangu kwako unikubali kama tambiko ya jioni.
3Ee Mwenyezi-Mungu ukilinde kinywa changu,
uweke ulinzi mlangoni mwa mdomo wangu.
4Unikinge nisielekee kufanya mabaya,
nisijishughulishe na matendo maovu;
nisijiunge na watu watendao mabaya,
wala nisishiriki kamwe karamu zao.
5Afadhali mtu mwema anipige kunionya;
lakini sikubali kamwe kusifiwa na wabaya,
maana nasali daima dhidi ya maovu yao.#141:5-7 maana katika Kiebrania si dhahiri.
6Wakuu wao watakapopondwa miambani,
ndipo watatambua maneno yangu yalikuwa sawa.
7Mifupa yao itatawanywa mdomoni pa Kuzimu
kama kuni zilizopasuliwa vipandevipande!
8Bali mimi nakutegemea, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu;
ninakimbilia usalama kwako, usiniache hatarini.
9Unikinge na mitego waliyonitegea,
uniepushe na matanzi ya hao watu waovu.
10Waovu wanaswe katika mitego yao wenyewe,
wakati mimi najiendea zangu salama.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 141: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia