Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 140

140
Sala ya kuomba ulinzi wa Mungu
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, uniokoe na watu wabaya,
unikinge na watu wakatili.
2Watu hao huwaza mabaya daima,
huzusha magomvi kila mara.
3 # Taz Rom 3:13 Ndimi zao hatari kama za nyoka;
midomoni mwao mna maneno ya sumu kama ya joka.
4Ee Mwenyezi-Mungu, unilinde na makucha ya wabaya;
unikinge na watu wakatili
ambao wamepanga kuniangusha.
5Wenye kiburi wamenitegea mitego,
wametandaza kamba kama wavu,
wameficha mitego njiani wanikamate.
6Namwambia Mwenyezi-Mungu, “Wewe ndiwe Mungu wangu.”
Usikilize, ee Mwenyezi-Mungu, sauti ya ombi langu.
7Ee Mwenyezi-Mungu, Bwana wangu, mkombozi wangu mkuu,
umenikinga salama wakati wa vita.
8Ee Mwenyezi-Mungu, usiwape waovu wanayotaka;
wala mipango yao mibaya usiifanikishe.
9Hao wanaonizingira wanainua vichwa;
uovu wa maneno yao uwapate wao wenyewe!
10Makaa ya moto yawaangukie;
watumbukizwe mashimoni, wasiinuke tena.
11Wanaowasengenya wengine wasifanikiwe katika nchi;
uovu uwapate wakatili na kuwaangamiza mara!
12Najua Mwenyezi-Mungu hutetea kisa cha wanaoteswa,
na kuwapatia haki maskini.
13Hakika waadilifu watalisifu jina lako;
wanyofu watakaa kwako.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 140: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia