Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 142

142
Dua ya mtu aliyeachwa mpweke
(Utenzi wa Daudi alipokuwa pangoni. Sala)
1Namlilia Mwenyezi-Mungu kwa sauti,
namsihi Mwenyezi-Mungu kwa sauti yangu.
2Namwekea malalamiko yangu,
namweleza taabu zangu.
3Ninapokaribia kukata tamaa kabisa,
yeye yupo, anajua mwenendo wangu.
Maadui wamenitegea mitego njiani mwangu.
4Nikiangalia upande wa kulia na kungojea,
naona hakuna mtu wa kunisaidia;
sina tena mahali pa kukimbilia,
hakuna mtu anayenijali.
5Nakulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu!
Wewe ni kimbilio langu la usalama;
wewe ni riziki yangu kuu katika nchi ya walio hai.
6Usikilize kilio changu, maana nimekuwa hoi;
uniokoe na watesi wangu, maana wamenizidi nguvu.
7Unitoe humu kifungoni,
ili nipate kukushukuru.
Watu waadilifu watajiunga nami
kwa sababu umenitendea mema mengi.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 142: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha