Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 62:1-5

Isaya 62:1-5 BHN

Kwa ajili ya Siyoni sitakaa kimya, kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, mpaka kuokolewa kwake kuchomoze kama umeme, wokovu wake utokeze kama mwenge. Mataifa watauona wokovu wako, wafalme wote watauona utukufu wako. Nawe utaitwa kwa jina jipya, jina atakalokupa Mwenyezi-Mungu mwenyewe. Utakuwa taji zuri mkononi mwa Mwenyezi-Mungu; kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako. Hutaitwa tena: “Aliyeachwa”, wala nchi yako haitaitwa: “Ukiwa”. Bali utaitwa: “Namfurahia,” na nchi yako itaitwa: “Aliyeolewa.” Maana Mwenyezi-Mungu amependezwa nawe, naye atakuwa kama mume wa nchi yako. Maana kama kijana mwanamume amwoavyo msichana, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi afurahivyo juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.

Soma Isaya 62