Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 2:12-22

Isaya 2:12-22 BHN

Naam, yaja siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi dhidi ya wenye kiburi na majivuno, dhidi ya wote wanaojikweza; dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni, ambayo ni mirefu na mizuri, dhidi ya mialoni yote nchini Bashani; dhidi ya milima yote mirefu, dhidi ya vilima vyote vya juu; dhidi ya minara yote mirefu, dhidi ya kuta zote za ngome; dhidi ya meli zote za Tarshishi, na dhidi ya meli zote nzuri. Kiburi chote cha watu kitakomeshwa, majivuno ya kila mtu yatavunjwa. Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo. Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa. Ingieni katika mapango miambani, katika mashimo ardhini, kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu, mbali na utukufu wa enzi yake, atakapokuja kuitia hofu dunia. Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo vinyago vyao vya fedha na dhahabu walivyojitengenezea ili kuviabudu. Nao wataingia katika mapango miambani na kwenye nyufa za miamba, kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu, mbali na utukufu wa enzi yake, atakapokuja kuitia hofu dunia. Usimwamini binadamu, uhai wake haudumu kama pumzi. Yeye anafaa kitu gani?

Soma Isaya 2