Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 2:12-22

Isaya 2:12-22 NEN

BWANA Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi, kwa wote wanaojikweza (nao watanyenyekezwa), kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana, na mialoni yote ya Bashani, kwa milima yote mirefu na vilima vyote vilivyoinuka, kwa kila mnara ulio mrefu sana na kila ukuta wenye ngome, kwa kila meli ya biashara, na kila chombo cha baharini cha fahari. Majivuno ya mwanadamu yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa, BWANA peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo, nazo sanamu zitatoweka kabisa. Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba, na kwenye mahandaki ardhini kutokana na utisho wa BWANA na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia. Siku ile, watu watawatupia panya na popo sanamu zao za fedha na za dhahabu, walizozitengeneza ili waziabudu. Watakimbilia kwenye mapango miambani na kwenye nyufa za miamba kutokana na utisho wa BWANA na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia. Acheni kumtumainia mwanadamu, ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake. Yeye ana thamani gani?