Kutoka 24:13-15
Kutoka 24:13-15 BHN
Basi, Mose akaondoka pamoja na Yoshua, mtumishi wake, akaenda kwenye mlima wa Mungu. Mose aliwaambia wale wazee, “Tungojeni hapa mpaka tutakapowarudia. Aroni na Huri wako pamoja nanyi; yeyote aliye na tatizo na awaendee wao.” Basi, Mose akaenda mlimani, na wingu likaufunika mlima.