Zaburi 89:29-33
Zaburi 89:29-33 SRUV
Wazao wake nao nitawadumisha milele, Na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu. Wanawe wakiiacha sheria yangu, Wasiende katika hukumu zangu, Wakizivunja amri zangu, Wasiyashike maagizo yangu, Basi, nitawarudi makosa yao kwa fimbo, Na uovu wao kwa mapigo. Lakini fadhili zangu sitamwondolea yeye, Wala sitafanya uaminifu wangu kuwa uongo.