Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 34:7-14

Zaburi 34:7-14 SRUV

Malaika wa BWANA huwazungukia, Wamchao na kuwaokoa. Onjeni muone ya kuwa BWANA yu mwema; Heri mtu yule anayemtumainia. Mcheni BWANA, enyi watakatifu wake, Maana, wamchao hawapungukiwi kitu. Wanasimba hutindikiwa, na kuona njaa; Bali wamtafutao BWANA hawapungukiwi kitu chochote kilicho chema. Njoni, enyi wana, mnisikilize, Nami nitawafundisha kumcha BWANA. Ni nani atamaniye uzima na atakaye kuishi, Siku nyingi afurahie mema? Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila. Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie.

Soma Zaburi 34

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 34:7-14