Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 33:10-22

Zaburi 33:10-22 SRUV

BWANA huyabatilisha mashauri ya mataifa, Huitangua mipango ya watu. Shauri la BWANA lasimama milele, Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi. Heri taifa ambalo BWANA ni Mungu wao, Watu aliowachagua kuwa urithi wake. Toka mbinguni BWANA huchungulia, Huangalia na kuwaona wanadamu wote. Akiwa katika kiti chake cha enzi. Huwaangalia wote wakaao duniani. Yeye aiumbaye mioyo yao wote Na kuziona kazi zao zote. Mfalme haokolewi kwa jeshi lake kubwa, Wala shujaa haokoki kwa kuwa na nguvu nyingi. Farasi hafai kitu kwa wokovu, Wala hamponyi mtu kwa wingi wa nguvu zake. Tazama, jicho la BWANA li kwao wamchao, Wazingojeao fadhili zake. Ili kuwaponya nafsi zao kutoka kwa mauti, Na kuwahuisha wakati wa njaa. Nafsi zetu zinamngoja BWANA; Yeye ndiye msaada wetu na ngao yetu. Maana mioyo yetu itamfurahia, Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu. Ee BWANA, fadhili zako zikae nasi, Kama tunavyo kutumainia Wewe.

Soma Zaburi 33

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 33:10-22

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha