Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 33:10-22

Zaburi 33:10-22 NEN

BWANA huzuia mipango ya mataifa, hupinga makusudi ya mataifa. Lakini mipango ya BWANA inasimama imara milele, makusudi ya moyo wake kwa vizazi vyote. Heri taifa ambalo BWANA ni Mungu wao, watu ambao aliwachagua kuwa urithi wake. Kutoka mbinguni BWANA hutazama chini na kuwaona wanadamu wote; kutoka maskani mwake huwaangalia wote wakaao duniani: yeye ambaye huumba mioyo yao wote, ambaye huangalia kila kitu wanachokitenda. Hakuna mfalme aokokaye kwa ukubwa wa jeshi lake; hakuna shujaa aokokaye kwa wingi wa nguvu zake. Farasi ni tumaini la bure kwa wokovu, licha ya nguvu zake nyingi, hawezi kuokoa. Lakini macho ya BWANA yako kwa wale wamchao, kwa wale tumaini lao liko katika upendo wake usio na kikomo, ili awaokoe na mauti, na kuwahifadhi wakati wa njaa. Sisi tunamngojea BWANA kwa matumaini, yeye ni msaada wetu na ngao yetu. Mioyo yetu humshangilia, kwa maana tunalitumainia jina lake takatifu. Upendo wako usio na mwisho ukae juu yetu, Ee BWANA, tunapoliweka tumaini letu kwako.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 33:10-22

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha