Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 40:15-24

Ayubu 40:15-24 SRUV

Mwangalie huyo kiboko, niliyemwumba pamoja nawe; Yeye hula nyasi kama ng'ombe, Tazama basi, nguvu zake zimo katika viuno vyake, Na uwezo wake u katika mishipa ya tumbo lake. Yeye hutikisa mkia wake mfano wa mwerezi; Mishipa ya mapaja yake yanaungamana pamoja. Mifupa yake ni kama mirija ya shaba; Mbavu zake ni kama vipande vya chuma. Yeye ni wa kwanza kwa hayo matendo makuu ya Mungu; Ni Muumba wake tu awezaye kumkabili kwa upanga wake. Hakika milima humtolea chakula; Hapo wachezapo wanyama pori wote. Hulala chini ya miti yenye vivuli, Mafichoni penye mianzi, na matopeni. Hiyo miti yenye vivuli humfunika kwa vivuli vyao; Mierebi ya vijito humzunguka. Tazama, mto ukifurika, yeye hatetemeki; Hujiona yu salama, ijapokuwa Yordani hufurika hata kinywani pake. Je! Mtu yeyote atamnasa akiwa yu macho, Au, kumtoboa pua yake kwa mtego?

Soma Ayubu 40