Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 3:1-10

Ayubu 3:1-10 SRUV

Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. Ayubu akajibu, na kusema; Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto wa kiume ametungishwa mimba. Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie. Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe. Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi. Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe. Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo Lewiathani. Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone mapambazuko; Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni.

Soma Ayubu 3