Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 3:1-10

Ayubu 3:1-10 NEN

Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake. Kisha akasema: “Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’ Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie. Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake. Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote. Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake. Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani. Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko, kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.