Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayu 3:1-10

Ayu 3:1-10 SUV

Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. Ayubu akajibu, na kusema; Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba. Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie. Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe. Tena usiku huo, na ushikwe na giza kuu; Usihesabiwe katika siku za mwaka; Wala kutiwa katika hesabu ya miezi. Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe. Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani. Nyota za mapambazuko yake na ziwe giza; Na utafute mwanga lakini usiupate; Wala usiyaone makope ya asubuhi; Kwa sababu haukuifunga milango ya tumbo la mamangu. Wala kunifichia taabu machoni.

Soma Ayu 3

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha