Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kumbukumbu la Torati 8:2-6

Kumbukumbu la Torati 8:2-6 SRUV

Nawe utaikumbuka njia ile yote BWANA, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arubaini katika jangwa, ili akunyenyekeze, kukujaribu kuyajua yaliyo moyoni mwako, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakunyenyekeza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA. Mavazi yako hayakuchakaa, wala mguu wako haukuvimba, miaka hiyo arubaini. Nawe fikiri moyoni mwako, ya kuwa kama vile baba amrudivyo mwanawe, ndivyo BWANA, Mungu wako, akurudivyo. Nawe uzishike amri za BWANA, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.

Video for Kumbukumbu la Torati 8:2-6