Zab 143:8-11
Zab 143:8-11 SUV
Unifanye kusikia fadhili zako asubuhi, Kwa maana nimekutumaini Wewe. Unijulishe njia nitakayoiendea, Kwa maana nakuinulia nafsi yangu. Ee BWANA, uniponye na adui zangu; Nimekukimbilia Wewe, unifiche. Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, Kwa maana ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa, Ee BWANA, unihuishe kwa ajili ya jina lako, Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni