Mit 28:1-5
Mit 28:1-5 SUV
Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu; Bali wenye haki ni wajasiri kama simba. Kwa sababu ya maasi ya nchi wakuu wake huwa wengi; Bali kwa wenye ufahamu na maarifa hali ya nchi hudumishwa Mtu mhitaji awaoneaye maskini, Ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza chakula. Wao waiachao sheria huwasifu waovu; Bali wao waishikao hushindana nao. Watu wabaya hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao BWANA huelewa na yote.