na Wapathrusi, na Wakasluhi; huko ndiko walikotoka Wafilisti, na Wakaftori. Na Kanaani akamzaa Sidoni, mwanawe wa kwanza, na Hethi; na Myebusi, na Mwamori, na Mgirgashi; na Mhivi, na Mwarki, na Msini; na Mwarvadi, na Msemari, na Mhamathi.
Wana wa Shemu; Elamu, na Ashuru, na Arfaksadi, na Ludi, na Aramu, na Usi, na Huli, na Getheri, na Mashi. Na Arfaksadi akamzaa Sala, na Sala akamzaa Eberi. Na Eberi akazaliwa wana wawili wa kiume; jina la wa kwanza aliitwa Pelegi, maana katika siku zake nchi iligawanyika; na jina la nduguye aliitwa Yoktani. Na Yoktani akamzaa Almodadi, na Shelefu, na Hasarmawethi, na Yera; na Hadoramu, na Uzali, na Dikla; na Obali, na Abimaeli, na Sheba; na Ofiri, na Havila, na Yobabu. Hao wote ndio wana wa Yoktani.
Shemu, na Arfaksadi, na Sala; na Eberi, na Pelegi, na Reu; na Serugi, na Nahori, na Tera; na Abramu, naye ndiye Ibrahimu.
Wana wa Ibrahimu; Isaka, na Ishmaeli.
Hivi ndivyo vizazi vyao; mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, Nebayothi; kisha Kedari, na Abdeeli, na Mibsamu; na Mishma, na Duma, na Masa, na Hadadi, na Tema; na Yeturi, na, Nafishi, na Kedema. Hao ndio wana wa Ishmaeli.
Na wana wa Ketura, suria yake Ibrahimu; yeye akamzaa Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani, na Ishbaki, na Shua. Na wana wa Yokshani; Sheba na Dedani.