Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zekaria 9:14-17

Zekaria 9:14-17 NENO

Kisha BWANA atawatokea; mshale wake utamulika kama radi. BWANA Mwenyezi atapiga tarumbeta, naye atatembea katika tufani za kusini, na BWANA wa majeshi atawalinda. Wataangamiza na kushinda kwa mawe ya kutupa kwa kombeo. Watakunywa na kunguruma kama waliolewa mvinyo; watajaa kama bakuli linalotumika kunyunyizia kwenye pembe za madhabahu. BWANA Mungu wao atawaokoa siku hiyo kama kundi la watu wake. Watangʼara katika nchi yake kama vito vya thamani kwenye taji. Jinsi gani watavutia na kuwa wazuri! Nafaka itawastawisha vijana wanaume, nayo divai mpya vijana wanawake.