Zaburi 95
95
Zaburi 95
Wimbo wa kumsifu Mwenyezi Mungu
1Njooni, tumwimbie Mwenyezi Mungu kwa furaha;
tumfanyie kelele za shangwe
Mwamba wa wokovu wetu.
2Tuje mbele zake kwa shukrani,
tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.
3Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni Mungu mkuu,
mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4Mkononi mwake mna vilindi vya dunia,
na vilele vya milima ni mali yake.
5Bahari ni yake, kwani ndiye aliyeifanya,
na mikono yake iliumba nchi kavu.
6Njooni, tusujudu, tumwabudu,
tupige magoti mbele za Mwenyezi Mungu Muumba wetu,
7kwa maana yeye ndiye Mungu wetu,
na sisi ni watu wa malisho yake,
kondoo chini ya utunzaji wake.
Mkiisikia sauti yake leo,
8msiifanye mioyo yenu migumu
kama mlivyofanya kule Meriba#95:8 maana yake Kugombana,
kama mlivyofanya siku ile
kule Masa#95:8 maana yake Kujaribiwa jangwani,
9ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima,
ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu.
10Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile,
nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka,
nao hawajazijua njia zangu.”
11Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu,
“Kamwe hawataingia rahani mwangu.”
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 95: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fsw.png&w=128&q=75)
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.