Zaburi 82
82
Zaburi 82
Maombi kwa ajili ya kutaka haki
Zaburi ya Asafu.
1Mungu anaongoza kusanyiko kuu,
anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”:
2“Hata lini utaendelea kuwatetea wasio haki
na kuonesha upendeleo kwa waovu?
3Teteeni wanyonge na yatima,
tunzeni haki za maskini na waliodhulumiwa.
4Mwokoeni mnyonge na mhitaji,
wakomboeni kutoka mkononi mwa mwovu.
5“Hawajui lolote, hawaelewi lolote.
Wanatembea gizani;
misingi yote ya dunia imetikisika.
6“Nilisema, ‘Ninyi ni “miungu”;
ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Sana.’
7Lakini mtakufa kama wanadamu wa kawaida;
mtaanguka kama mtawala mwingine yeyote.”
8Ee Mungu, inuka uihukumu nchi,
kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 82: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.