Zaburi 83
83
Zaburi 83
Maombi kwa ajili ya kushindwa kwa adui za Israeli
Wimbo. Zaburi ya Asafu.
1Ee Mungu, usikae kimya,
usinyamaze, Ee Mungu, usikae mbali.
2Tazama watesi wako wanafanya fujo,
jinsi adui zako wanavyoinua vichwa vyao.
3Kwa ujanja, wanapanga njama dhidi ya watu wako;
wanapanga hila dhidi ya wale unaowapenda.
4Wanasema, “Njooni, tuwaangamize kama taifa,
ili jina la Israeli lisikumbukwe tena.”
5Kwa nia moja wanapanga njama pamoja,
wanafanya muungano dhidi yako,
6mahema ya Edomu na Waishmaeli,
ya Wamoabu na Wahagari,
7Gebali#83:7 yaani Bubilo, Amoni na Amaleki,
Ufilisti, pamoja na watu wa Tiro.
8Hata Ashuru wameungana nao
kuwapa nguvu wazao wa Lutu.
9Uwatendee kama vile ulivyowatendea Midiani,
na kama vile ulivyowatendea Sisera na Yabini
hapo kijito cha Kishoni,
10ambao waliangamia huko Endori
na wakawa kama kinyesi juu ya ardhi.
11Wafanye wakuu wao kama Orebu na Zeebu,
watawala wao kama Zeba na Salmuna,
12ambao walisema, “Na tumiliki maeneo
ya malisho ya Mungu.”
13Ee Mungu wangu, wapeperushe kama mavumbi ya kisulisuli,
kama makapi yapeperushwayo na upepo.
14Kama vile moto unavyoteketeza msitu
au mwali wa moto unavyounguza milima,
15wafuatilie kwa tufani yako
na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16Funika nyuso zao kwa aibu
ili watu walitafute jina lako, Ee Mwenyezi Mungu.
17Wao na waaibishwe na kufadhaishwa milele,
na waangamie kwa aibu.
18Hebu wajue kuwa wewe, ambaye jina lako ni Mwenyezi Mungu,
kwamba wewe peke yako ndiwe Uliye Juu Sana ya dunia yote.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 83: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.