Zaburi 68:19-23
Zaburi 68:19-23 NENO
Ahimidiwe Bwana, Mungu Mwokozi wetu, ambaye siku kwa siku hutuchukulia mizigo yetu. Mungu wetu ni Mungu anayeokoa, Bwana Mungu Mwenyezi hutuokoa na kifo. Hakika Mungu ataponda vichwa vya adui zake, vichwa vya hao wanaoenda katika njia za dhambi. Bwana alisema, “Nitawarudisha kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari, ili uweze kuchovya miguu yako katika damu ya adui zako, huku ndimi za mbwa wako zikiwa na fungu lake.”