Zaburi 67
67
Zaburi 67
Mataifa wahimizwa kumsifu Mwenyezi Mungu
Kwa mwimbishaji. Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi. Wimbo.
1Mungu aturehemu na kutubariki,
na kutuangazia nuru za uso wake,
2ili njia zako zijulikane duniani,
wokovu wako katikati ya mataifa yote.
3Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
4Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe,
kwa kuwa unatawala watu kwa haki
na kuongoza mataifa ya dunia.
5Ee Mungu, mataifa na wakusifu,
mataifa yote na wakusifu.
6Ndipo nchi itatoa mazao yake,
naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.
7Mungu atatubariki
na miisho yote ya dunia itamcha yeye.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 67: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
![None](/_next/image?url=https%3A%2F%2Fimageproxy.youversionapi.com%2F58%2Fhttps%3A%2F%2Fweb-assets.youversion.com%2Fapp-icons%2Fsw.png&w=128&q=75)
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.