Zaburi 32:1-3
Zaburi 32:1-3 NEN
Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake, ambaye dhambi zake zimefunikwa. Heri mtu yule ambaye BWANA hamhesabii dhambi, na ambaye rohoni mwake hamna udanganyifu. Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.