Zaburi 19
19
Zaburi 19
Utukufu wa Mwenyezi Mungu katika uumbaji
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Mbingu zinatangaza utukufu wa Mungu,
anga zahubiri kazi ya mikono yake.
2Siku baada ya siku zinatoa habari,
usiku baada ya usiku zinatangaza maarifa.
3Hakuna msemo wala lugha,
ambapo sauti zao hazisikiki.
4Sauti yao imeenea duniani pote,
nayo maneno yao yameenea
hadi miisho ya ulimwengu.
Katika mbingu amepiga hema kwa ajili ya jua,
5linafanana na bwana arusi
akitoka chumbani mwake,
kama shujaa anavyofurahia
kukamilisha kushindana kwake.
6Huchomoza upande mmoja wa mbingu,
na kufanya mzunguko wake
hadi upande mwingine.
Hakuna kilichojificha joto lake.
7Torati ya Mwenyezi Mungu ni kamilifu,
ikihuisha nafsi.
Shuhuda za Mwenyezi Mungu ni za kuaminika,
zikimpa mjinga hekima.
8Maagizo ya Mwenyezi Mungu ni kamili,
nayo hufurahisha moyo.
Amri za Mwenyezi Mungu huangaza,
zatia nuru machoni.
9Kumcha Mwenyezi Mungu ni utakatifu,
nako kwadumu milele.
Amri za Mwenyezi Mungu ni za hakika,
nazo zina haki.
10Ni za thamani kuliko dhahabu,
kuliko dhahabu iliyo safi sana,
ni tamu kuliko asali,
kuliko asali kutoka sega.
11Kwa hizo mtumishi wako anaonywa,
katika kuzishika kuna thawabu kubwa.
12Ni nani awezaye kutambua makosa yake?
Nisamehe makosa yangu nisiyoyajua.
13Mlinde mtumishi wako na dhambi za makusudi,
nazo zisinitawale.
Ndipo nitakapokuwa sina lawama,
niwe huru na hatia kubwa.
14Maneno ya kinywa changu
na mawazo ya moyo wangu,
yapate kibali mbele zako, Ee Mwenyezi Mungu,
Mwamba wangu na Mkombozi wangu.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 19: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili
Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.