Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 114

114
Zaburi 114
Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri
1 Wakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
3 Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 114: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia