Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 114

114
Zaburi 114
Maajabu Ya Mungu Wakati Israeli Walipotoka Misri
1 Wakati Israeli walipotoka Misri,
nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu,
Israeli akawa milki yake.
3 Bahari ilitazama ikakimbia,
Yordani ulirudi nyuma,
4 milima ilirukaruka kama kondoo dume,
vilima kama wana-kondoo.
5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia,
nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume,
enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana,
mbele za Mungu wa Yakobo,
8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji,
mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 114: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha